TOPBAND

TOPBAND

Saturday, May 8, 2010

HASHIM THABEET AMENIPiGA.

Ilikua majira ya saa kumi unusu nikiwa natoka club billcanas pamoja na rafiki yangu ANNA tukiongozana kuelekea mlango mkubwa wa kioo nikiwa naongea na simu na Hisbert kwa sauti ya juu maana kelele za muziki zilikua zinasumbua nikiwa nimesimama nje ya mlango wa kioo ghafla akatokea bwana HASHIM ambaye alikua counter akiongea na wakata ticket akaja nje na kunipiga bonge la mtama nikaaunga chini ya sakafu na kuzirai kwa dakika kadhaa,mabaunsa wakanibeba na kuniweka pembeni maana nilikua mlangoni,nilipozinduka nilisikia maumivu makali kwenye mabega,mkono wangu wa kulia na mguu ambao unafanya kutembea kwangu kwa taabu,nikaangalia mkononi simu yangu sikuiona tena,nikawauliza mabaunsa wake jamaa amekwenda wapi!wakadai ameondoka tayari...nikajikokota kuelekea kwenye gari yangu na kuelekea polisi kutoa taarifa niweze kupata matibabu,nilipofika nikaaandika statement nikapewa namba ya case CD/RB/6848/10 pia nikapatiwa PF3 nikaenda hospitali nikapata matibabu,sasa hivi niko kitandani siwezi kutembea vizuri,pia nitashindwa kuperfom kwenye harusi ambayo tayari nishalipwa pesa tayari.SWALI langu ni kwanini ameamua kunidhalilisha vile mbele ya CLUB na FANZ ambao nilikua nawatumbuiza?kwanini ameamua kuniharibia kazi yangu?kwanini ameamua kunipiga bila ya kumkosea?JE NI SAWA HIVI JAMANI....naona  MACHOZI YANANITOKA SINA CHA KUMUELEZA MAMA YANGU.

11 comments:

  1. ilikua lini hiyo TID?manake sidhani kama kesi ilikua kubwa kiasi ya yeye kuweza kukurupuka nakukuumiza!!!
    inatia aibu mmmno

    ReplyDelete
  2. Ebwana pole sana TID lakini kwa jinsi ninavyomfaham HASHEEM Hawezi kukurupuka tu hakakufanyia hivyo hata kidogo hiyo haiwezekani,na kwa jinsi tunavyokujua weye lazima kuna kitu umemfanyia trust me,Hasheem bonge ya mshkaji na hana mambo ya kishamba but u do ndo mana kutakuwa na kitu hapa,mshkaji anatuwakirisha level zile jamani East Africa yote tunajivunia kuwa na Hasheem-A plus(jina langu)

    ReplyDelete
  3. This comment has been removed by the author.

    ReplyDelete
  4. Ebana pole sana ndio ukubwa huo, ila kama anavyosema jama hapo juu Hasheem mshkaji na nimpenda watu, lazima itakuwa kuna kitu kimejifisha hapo ila kaa uzingatie, kwani ugovi haujengi na nitabia mbaya katika jamii,fikiria sana na lazinma ujuwe chanzo nikitugani, maana kama kupikwa mtama ukiangalia Hasheem Ni NBA Basketball sidhani kama anatumia sana miguu kama mcheza soccer, Muhemu nikutafuta suluhisho kwani nyote mnaangaliwa katika jamii hii ya sasa Big time.

    ReplyDelete
  5. we fala acha uongo..... we mtoto wa kiume utapigwaje mtama kesho ushindwe kuamka... we msenge nn, una lolote sema sahivi umefulia unatafuta umaarufu kwa nguvu. mtoto wakiume sio kila kitu unakimbilia police, ata dem wako anakuona kunguru fala wewe.... tena usiongee mbele za watu utachekwa

    ReplyDelete
  6. dah brother ndo maisha hayo u cant battle wit a dude who is paid over 6 billion shillings per year...kubali tu brother hasheem does not belong to your world...he belongs to another world kaka mkubwa..your fighting with a great wall of china....lakini kaka tumesikia demu wako kamshobokea jamaa its obvious lazima amshobokee coz jamaa is so paid!!! pole dude dats challenge...we ka vipi ipotezeeee masuala ya kufungua kesi ya kishamba utapoteza tu energy the police cant do nuthn to dat dude...unalijua hilo. peace

    ReplyDelete
  7. wageni wako nyumbani kwako wote wapo agaist you why???? hilo ni swali la kujiuliza bru they is something wrong to you iam not saing that coz i wasnt there lakini kwa kusoma habari tofauti kutoka ktk blog mbali mbali na magazeti kila mmoja anakubandikia lawama sijui kwa nini next time take ezy hata kama demu kamshobokea jamaa unakula bati kiume tu wangapi wazuri by the way karibu sana tena cape town we miss you may be ilikuwa mipombe bado i like you are music man good luck

    ReplyDelete
  8. Pole T.I.D ila siyo mpango the way you both acted, act like gentlmen guyz

    ReplyDelete
  9. Mhm pole TID...mi naitwa nina na sie tunaemjua TID kwakweli hatushangai kwa hili hata kidogo,nilikuwepo pale club siku ile na nashangaa sana kuona TID ameandika uongo huo kwamba anashangaa kwanini amezalilishwa kiasi kile?kwa jinsi alivyomfanyia hasheem hata ingekuwa mitume,malaika wasingeweza vumilia..hasheem ni mtu mpenda watu,hana nyodo nyodo kama za TID,mi nazani frustration za muziki zimechangia,TID jaribu tembelea www.hasheemthabeet.com sio blog spot ni website,jamani nimemaliza,mi ni jirani yake TID kinondoni.

    ReplyDelete
  10. Mhm pole TID...mi naitwa nina na sie tunaemjua TID kwakweli hatushangai kwa hili hata kidogo,nilikuwepo pale club siku ile na nashangaa sana kuona TID ameandika uongo huo kwamba anashangaa kwanini amezalilishwa kiasi kile?kwa jinsi alivyomfanyia hasheem hata ingekuwa mitume,malaika wasingeweza vumilia..hasheem ni mtu mpenda watu,hana nyodo nyodo kama za TID,mi nazani frustration za muziki zimechangia,TID jaribu tembelea www.hasheemthabeet.com sio blog spot ni website,jamani nimemaliza,mi ni jirani yake TID kinondoni.

    ReplyDelete
  11. Pole na Mizozo kaka,
    Ningependa kaka hasira ulizonazo kwa sasa uzihamishie kwenye kazi yako ya Muziki.Ni kweli mtu mzima unapodhalilishwa inauma ila huna namna imesha tokea kaka.
    Ukiwa kama mwanamuziki uliye na jina ingekuwa busara kwa wakati huu kukaa chini na kuamua kabisa kufanya mambo makubwa ktk fani.
    Kuteleza sio kuanguka kaka.Wengi watasema lakini kumbuka umri nao unakimbia.Ni muda muafaka kujikita kwenye kazi yako hii na kulikuza ndani na nje ya nchi jina lako na bendi yako.
    Ajali kama hizi ni za kawaida kwenye maisha ila ni kujaribu kuzipunguza kwan hamna aliyekamilika.Pia muwe mnaangalia mbele zaidi na kufikiria zaidi mambo makubwa kuliko kulewa na vijisifa hivi tunavyowapa.
    Kumbuka ulikuja kivingine kabisa ulivyotoka jela na unaweza kabisa kuendeleza mot ule ukawa juu daima.
    Pia kuwa makini sana na marafiki wanaokuzunguka wengine wako kwa ajili ya maslahi yao UKIYUMBA wanakimbia.
    Kaka ..kaka..muda ndio huu wao wameweza kwanini wewe ushindwe.

    Kaza buti

    ReplyDelete